Sehemu ya Tafsiri na Ukalimani

Majukumu ya Sehemu hii ni:-

  1. Kutoa huduma za tafsiri na ukalimani  ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
  2. Kuratibu na kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa ajili ya kujenga na kuimarisha uwezo wa wafasiri na wakalimani kitaifa na kimataifa;
  3. Kuandika makala na maandiko mengine yanayohusiana na tafsiri na ukalimani;
  4. Kuandaa na kuhuisha kanzidata ya wafasiri na wakalimani ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa lengo la kuwakutanisha na fursa pindi zinapotokea;
  5. Kuthibiti ubora wa kazi za tafsiri na ukalimani;
  6. Kupitia na kuthibitisha tafsiri zilizofanywa na taasisi zingine na mawakala wa BAKITA; na
  7. Kufanya tafiti  zinazohusiana na tafsiri na ukalimani.