Sehemu ya Istilahi na Kamusi
Majukumu ya Sehemu hii ni: -
- Kuandaa msamiati na istilahi zinazotakiwa kusanifishwa, kuratibu usanifishaji wake na kuzisambaza;
- Kuandika kamusi za jumla na mahususi kwa ajili ya matumizi ya taaluma mbalimbali;
- Kufanya utafiti kuhusiana na kamusi na istilahi mbalimbali;
- Kuandika makala na maandiko mengine kuhusiana na kamusi na istilahi; Kutoa mafunzo ya muda mfupi ya uandaaji wa kamusi na istilahi kwa wanaohitaji; na
- Kukusanya maneno kutoka kwenye maandiko ya Kiswahili na kuyaingiza kwenye Kongoo ya Kiswahili ya Taifa.
