Sehemu ya Utumishi na Utawala
Majukumu ya Sehemu hii ni kama ifuatavyo: -
- Kutafsiri sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali ya huduma na kushauri utekelezaji wake;
- Kuandaa na kutoa mafunzo kwa watumishi;
- Kuandaa na kusimamia mishahara ya watumishi;
- Kusimamia mfumo wa usimamizi wa taarifa za kiutumishi na mishahara za wafanyakazi wa BAKITA
- Kusimamia mipango ya mafao na fidia kwa watumishi;
- Kuratibu uundaji na utendaji kazi wa Baraza la Wafanyakazi;
- Kusimamia masuala ya nidhamu mahali pa kazi;
- Kusimamia shughuli zote za kiutawala ofisini;
- Kutoa huduma na msaada wa kisheria;
- Kutunza nyaraka zote za kisheria za Baraza; na
- Kusimamia tafiti za kisheria na kuushauri vyema utawala wa Baraza.
