Sehemu ya Lugha, Fasihi na Uhariri

Majukumu ya Sehemu hii ni: -

  1. Kupitia na kutoa ithibati ya matumizi sahihi ya Kiswahili katika maandiko mbalimbali;
  2. Kutoa mafunzo ya Kiswahili kwa wageni;
  3. Kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa makundi yenye mahitaji  mbalimbali kuhusu lugha na fasihi ya Kiswahili;
  4. Kutoa mafunzo ya muda mfupi kuhusu mbinu za uandishi na uhariri kwa wanaohitaji.
  5. Kuandika makala na maandiko mengine kuhusu lugha na fasihi ya Kiswahili;
  6. Kufanya tafiti na kutoa machapisho kuhusu fasihi ya Kiswahili;
  7. Kuhariri vitabu, miswada na maandiko mengine ya Kiswahili;
  8. Kuandaa mashindano ya uandishi wa lugha ya Kiswahili katika ngazi mbalimbali za elimu;
  9. Kuendesha na kuratibu mafunzo kwa wanafunzi wanaofanya kazimradi zinazohusiana na lugha ya Kiswahili; na
  10. Kuratibu na kuendesha maonesho ya utamaduni.