Sehemu ya Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini
Majukumu ya Sehemu hii ni:-
- Kuratibu utayarishaji na utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Muda wa Kati, Mipango Kazi na Bajeti ya Mwaka kulingana na bajeti ya serikali;
- Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mipango ya Baraza;
- Kuandaa ripoti za utekelezaji wa miradi, programu mbalimbali, na mipango kazi;
- Kusimamia uandaaji na utekelezaji wa programu za uwekezaji za Baraza;
- Kufanya tathmini ya shughuli mbalimbali za Baraza; na
- Kuandaa na kutekeleza mikakati ya uhamasishaji wa matumizi ya rasilimali
