Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa kufanyika Paris Ufaransa Mwezi April 2026.
Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo ya Kiswahili Sanifu na Fasaha kwa Waandishi Waendesha Ofisi wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi (TAPSEA) Bi. Zuh
Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) ni Shirika la Umma ambalo kwa kawaida huwa chini ya Wizara yenye dhamana ya Utamaduni. Baraza liliundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 27 ya mwaka 1967 pamoja n
Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) ni Shirika la Umma ambalo kwa kawaida huwa chini ya Wizara yenye dhamana ya Utamaduni. Baraza liliundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 27 ya mwaka 1967 pamoja n
Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) ni Shirika la Umma ambalo kwa kawaida huwa chini ya Wizara yenye dhamana ya Utamaduni. Baraza liliundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 27 ya mwaka 1967 pamoja n
MAFUNZO YA KUIMARISHA STADI ZA KUFUNDISHA KISWAHILI KWA WAGENI
Ushuhuda.
"
Nimepata fursa ya kujifunza Kiswahili kwa miezi kadhaa BAKITA, jambo ambalo limeniwezesha kufanya kazi ya udaktari nchini Tanzania. Wakufunzi wa lugha wana ujuzi mkubwa na ni wakarimu katika kuwasaidia wanafunzi; kwa hakika timu ya mafunzo ni bora sana na hujitahidi zaidi ya kawaida kuhakikisha unapata ujuzi wa lugha na mawasiliano, pamoja na uwezo wa kutumia Kiswahili kitaaluma, kwa muda mfupi iwezekanavyo. Hivyo basi, ninalipendekeza BAKITA kwa mtu yeyote anayevutiwa kujifunza Kiswahili.
Dkt. Augustine Balaara
Mjifunzaji wa Kiswahili
"
Kama mjifunzaji wa lugha ya Kiswahili niliyekamilisha hatua ya awali lakini nikiwa na dhamira kubwa na hitaji la kufikia ufasaha kwa haraka, nimegundua kuwa kitabu cha kujifunzia “FURAHIA KISWAHILI” kimenisaidia sana. Kitabu hiki hakina masomo yenye thamani na maelezo rahisi kueleweka tu, bali pia kinamhimiza mwanafunzi kuchunguza na kufurahia lugha kikamilifu—ambayo ndiyo njia bora zaidi ya kujifunza. Muundo wa kitabu ni mpana na wa kina, kwani kinajumuisha kila kitu kuanzia maelezo ya sarufi na mazoezi ya kusikiliza hadi maelezo ya kitamaduni na muktadha wa matumizi. Ninapendekeza sana “FURAHIA KISWAHILI”; hakika kinatimiza kikamilifu maana ya jina lake.
Maja Schentz, Sweden
Mjifunzaji wa Kiswahili
"
Tangu siku niliyofahamishwa kuhusu BAKITA kupitia mtu niliyefahamiana naye, sijawahi hata mara moja kujuta kuchukua masomo yao. Nilikuwa na walimu wawili wazuri sana, waliokuwa na upole na uvumilivu mkubwa kwangu. Ingawa nilichagua kozi ya wiki sita, kiwango cha Kiswahili nilichojifunza kilinisaidia katika kipindi changu chote nchini Tanzania na mahali pangu pa kazi. Nilianza bila kujua chochote kuhusu lugha hii, lakini sasa ninaweza kuendesha mazungumzo kwa Kiswahili. Kwa kujiamini ninaweza kusema kuwa nimeongeza lugha nyingine moja katika orodha ya lugha ninazoweza kuzungumza na kuelewa.