Tanzania emblem

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania


Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA)

Tanzania emblem

Vitengo Mbalimbali vya BAKITA

Majukumu ya Kitengo hiki ni kama ifuatavyo:

  1. Kuandaa na kutekeleza mpango- mkakati wa TEHAMA
  2. Kutoa ushauri kuhusu matumizi sahihi ya teknolojia zenye gharamu naafu
  3. Kuandaa na kusimamia makavazi ya kielektroni kwa ajili ya kutunza nyaraka na kumbukumbu muhimu za Baraza
  4. Kutoa huduma endelevu za msaada kwa watumiaji
  5. Kuunda na kusimamia mifumo ya uhifadhi na urejeshaji wa data za Baraza
  6. Kushirikiana na Wakala wa Serikali Mtandao ili kuhakikisha uzingatiaji wa sera, sheria na viwango vya TEHAMA serikalini
  7. Kuandaa, kukusanya na kuhifadhi takwimu za Baraza

Majukumu ya kitengo hiki ni kama ifuatavyo;

Kushauri kuhusu masuala ya kuanzisha kazi/biashara mpya, kukuza mitandao na ushirikiano kwa wabia wa kitaifa na kimataifa na kuvutia wateja katika huduma zinazotolewa na Baraza.

  1. Kuanzisha na kutekeleza mikakati ya masoko;
  2. Kutangaza na kuuzabidhaa na huduma mbalimbali zinazotolewa na Baraza
  3. Kuhifadhi kumbukumbu za matukio yote ya Baraza
  4. Kupitia na kuhuisha taarifa katika tovuti na majukwaa ya mitandao yote ya kijamii
  5. Kupokea maswali, maombi na maoni kutoka kwa wadau mbalimbali
  6. Kufanya utafiti wa masoko ya bidhaa na huduma zinazotolewa na Baraza

Majukumu ya kitengo hiki ni kama ifuatavyo

  1. Kuandaa mpango wa ukaguzi wa ndani wa Baraza
  2. Kuunda na kusimamia utekelezaji wa sera za ukaguzi wa ndani
  3. Kupendekeza maboresho ya utendaji kazi wa ndani ya Baraza
  4. Kufanya ukaguzi wa ndani katika maeneo yote ya shughuli za Baraza
  5. Kushirikiana na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali wakati wa ukaguzi
  6. Kusimamia upatikanaji wa majibu ya hoja za ukaguzi.

Majukumu ya Kitengo hiki ni kama ifuatavyo:

  1. Kutunza kaseti, magazeti, video, na filamu za Kiswahili
  2. Kuwasaidia watafiti na wanafunzi wa lugha ya Kiswahili
  3. Kuandaa na kusimamia taarifa, sera na taratibu za maktaba
  4. Kuanzisha na kusimamia utumiaji wa Mfumo wa Taarifa za Maktaba pamoja na huduma zake

Kitengo cha Ununuzi na Ugavi

Majukumu ya Kitengo hiki ni kama ifuatavyo

  1. Kuandaa na kutekeleza mipango ya mwaka ya ununuzi na ugavi
  2. Kusimamia utekelezaji wa sheria na kanuni za ununuzi na ugavi Serikalini
  3. Kusimamia mchakato wa zabuni kwa kufuata taratibu zilizopo
  4. Kutoa taarifa za ununuzi za vipindi mbalimbali
  5. Kuandaa orodha ya vifaa vya ofisi